FANUEL SEDEKIA - "JINA LA YESU" SONG

Thursday, January 31, 2013

RACHEL SHARP AWAKUTANISHA WAANDISHI WA HABARI NA BLOGGERS KUTAMBULISHA ALBAMU YAKE NA KUZUNGUMZIA UMUHIMU WA KUTUMIA NYIMBO ZA ASILI ZA INJILI KUFIKISHA UJUMBE WA MUNGU KWA WATU WOTE


Mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania anaishi Sweden Rachel Sharp siku ya Jumamosi aliongea na waandishi wa habari na blogger nyumbani kwake Tegeta kuhusiana na ujio wake mpya wa albamu yake ya pili ya “NI MUNGU WA AJABU” ambayo iko katika mfumo wa audio na video.
Mwimbaji huyu kwa sasa anaishi nchini Sweden na ambako anafanaya huduma ya kumtangaza Kristo na ni majasiliamali.
Rachel Sharp
Rachel Sharp aliwahimiza watu kupenda utamaduni wao na kuachana na tabia ya kukopi tamaduni za watu. Alisisitiza sana kuwa kama Watanzania tunatakiwa kuwa na mfumo wetu wa uimbaji ambao utafanya watu wengine kuupenda kutamani kufanya kama sisi. Alisema “Watu wamekuwa wakipenda sana nyimbo za Afrika Kusini kuliko nyimbo za wazawa..tunatakiwa kubadilika”

Rachel Sharp alimshukuru sana Mungu wa hatua aliyofikia ya uimbaji kwani, alikotokani mbali sana.

Rachel kwa sasa ni mama mwenye watoto wawili wanaoishi nchini Sweden na ni mama aliolewa na mzungu wa Kiswedeni. Hivi sasa yuko nchini Tanzania kwa likizo fupi, na baada ya hapo atarudi nchini Sweden kwa majukumu mengine


Press release
KARIBUNI sana wanahabari katika hafla yetu hii fupi  yenye lengo la kumpa Mungu wetu utukufu. Mimi ninaitwa Rachel Scharp, ni Mwimbaji wa nyimbo za Injili, ninaishi Malmo Sweden. Lakini kwa sasa nipo nyumbani kwa ajili ya utambulisho wa Albamu yangu ya Mziki wa Injili.
Uimbaji kwangu ni maisha kwa kuwa nilianza kuupenda muziki na kuimba nikiwa mdogo sana, nilikuwa nikitunga nyimbo na kuwafundisha wadogo zangu. Tuliimba nyimbo  hizo jioni, haswa kwa kipindi kile cha ugawaji ikiwa zamu ya kwaya yetu, ile foleni ya kununua mchele iliyokuwa ndefu chakula kilikuwa kinachelewa, ili wadogo zangu wasilale bila kula na furaha ya kusubiria ubwabwa na maharage basi tunaimba kusubiria msosi. Wakati huo hakukuwa na TV kama ilivyo sasa.
Niliimba kwaya ya shule pale “Jangwani Secondary” pia niliongoza sifa na kuabudu kwenye Fellowship katika Kanisa la Msewe Lutheran. Nilikuwa nikiandika nyimbo nyingi nikitegemea kupata fursa ya kurekodi na kuimba na Kwaya nyimbo zangu, lakini sikupata fursa hiyo.
Kwa sasa ninaimba kwaya ya Kanisa la Elim Pentecostal huko Malmo Kusini mwa Sweden, ninaongoza sifa na kuabudu. Ninaimba pia kwenye kundi linaloitwa Shalom International ambalo ni muunganiko wa waimbaji kutoka makanisa mbali mbali ya Kiroho yaliyopo mjini Malmo. Nilipata fursa ya kurekodi albam yangu ya kwanza mwaka 2008 nikazinduliwa huko Sweden, Mei mwaka 2009 nikisindikizwa na dada Upendo Kilahiro. Albam hiyo niliita ‘Nalinga na Yesu’ yenye nyimbo 9, iko kwenye mfumo wa sauti tu.
Leo ninatambulisha album yangu ya Pili yenye jina la ‘Ni Mungu wa Ajabu’. Album hii ina nyimbo kumi zilizo kwenye mfumo wa sauti (audio), na 8 kwenye mfumo wa Picha na Sauti (DVD). Nimerekodi album hii Oktoba mwaka 2011 nchini Sweden, kwa upande wa mpangilio wa vyombo na muziki nikisaidiwa na Paalab Nyarko, kutoka Ghana na Producer Zillile Matikinga (Zorro) – kutoka South Afrika.
Mwanzoni mwa mwaka 2012 niliongeza na baadhi ya vionjo vya muziki kwenye studio za New Life Band Arusha, vionjo nilivyoingiza ni gitaa la solo lililopigwa na Godlucky Matingisa wa New Life Band Arusha, Base gitaa limepigwa na Wilson Godfrey Mtangoo. Ngoma zilipigwa na Fujo Makaranga. Na sauti pia niliingiza hapo Arusha nikisaidiwa na Jackson Benty, chini ya usimamizi na uangalizi wa Producer Wilson Mtangoo. Mwalimu wa sauti ni Mchungaji David Nkone.
Video imerekodiwa na UMU Production Arusha chini ya uongozi wa Jojo Jose Mwakajila. Video hii imerekodiwa Sweden (Malmo), Ujerumani (Berlin), Tanzania (Dar es Salaam, Bagamoyo, Arusha, Moshi, Serengeti).
Midundo ya nyimbo ni ya kiasili (kitamaduni). Napenda nyimbo zenye vionjo vya Kiafrika na Kitanzania zaidi. Nimeimba kwa Kiswahili na Kiingereza pia. Na nyimbo nyingi ni za Kiswahili, hii haimanishi kwamba soko liko nchi wanazoongea Kiswahili tu. Cha kushangaza ni kwamba pia nchi za Scandinavia wanapenda san Kiswahili na kukithamini, na nafikiri kuliko hata sisi wenye lugha.
Wanasema kwamba ni lugha yenye sauti tamu name sina budi kujivunia na kuiendeleza na huku nikimsifu Mungu na kupeleka ujumbe kwa watu wake.
Nyimbo hizi zimebeba ujumbe mbali mbali, kuna za kumsifu Mungu na matendo yake makuu, kuna za maonyo na kuna za kutia moyo kwa safari hii ngumu ya kwenda Mbinguni.
Ningependa sana watu wapate ujumbe huu na wakutane na Mungu katika maeneo hayo tofauti kama nilivyoeleza mwanzoni kuwa kuna kumsifu na kumwabudu Mungu, kuonywa na kutiwa moyo pia. Inategemea mtu yuko kwenye hali gani na ana mahitaji gani.
WITO WANGU KWA JAMII
Kwanza ni kupenda na kuthamini kile tulicho nacho Mungu alichotupatia. Kwanza kwa sisi wakristo tumepewa Neema hii ya wokovu tunatakiwa tuipende, tuithamini, tuitunze na tuiendeleze, tusiichezee na tuwafanye wengine pia waijue na waipate.
Kama tusipoipenda, tusipoithamini, kujivunia na kuilinda, wengine hawatajua thamani yake.
Nikija kwenye jamii yetu kwa sasa tunapenda sana  kuiga kutoka nje tunaacha ya kwetu, sikatai kuiga yale yaletayo maendeleo, na tunahitaji kujifunza kutoka kwa walioendelea, lakini si kwamba tuvipuuzie vya kwetu. Kuna vyetu vinavyohitaji mwendelezo. Na tene vikawa vizuri sana na wan je wakaiga kutoka kwetu. Kwa mfano; muziki wetu, lugha yetu na vingine vingi.
Kwa upande wa muziki, Watanzania siku hizi wanapenda sana muziki kutoka Afrika Kusin, ni mzuri sana hata mimi ninapendezwa nao. Naona sasa waimbaji wengi wanapenda kuiga mtindo huo. Ule ni muziki wa asili wa ngoma zao za kienyeji ukawekewa/ukaongezewa vionjo vya kisasa.
Sasa na sisi tutakapopiga mziki huo hautakuwa mzuri kama wanavyopiga Joyous Celebration kwa kuwa ndio asili yao. Swali ni kwamba, kwa nini sisi Watanzania tusitengeneze lizombe letu au Mdumange au Sindimba na hata Mdundiko tukaweka vionjo vya kisasa ukawa mzuri na wao waige kutoka kwetu? Nilazima tujitahidi jamani tuwe na utambulisho wetu (identity). Kwamba ukisikika muziki uutambue mmmh Huu ni muziki wa Tanzania, tunahitaji ubunifu tu kuondoa uvivu wa kufikiri. Kama tukitulia na kubuni na kutumia vipawa tulivyopewa na Mungu tutafika mbali sana na sio kupita njia ya mkato ya kuiga tu.
Ninamaliza kwa kuwaambia Watanzania, tusiende kwa mazoea eti watu wamezoea hivi. Huu ni wakati wa mabadiliko, tubadilike turudi kwetu. Tutafika mbali. Watanzania tunaweza, na kuleta mabadilikoni mimi na wewe.
Asanteni sana kwa kuja kushiriki pamoja name tukio hili la Baraka. Mungu awabariki sana.Rachel Scharp
 Rachel akicheza sawa na Bloggers Uncle Jimmy na Rulea Sanga.
 MC na mtangazaji wa Wapo Radio, Ritha Chiwalo akifanya utambulisho.
 Bloga Papa (kushoto) akiwa makini katika kazi ya urushaji habari mitandaoni, anayefuatia ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania, Upendo Kilahiro akiwa na mwanae.
 Master Prophet Machibya akitambulishwa na MC Ritha Chiwalo
 MC Chiwalo akimsikiliza mtoto wa Upendo Kilahiro akijitambulisha akiwa na mtoto wake Ritha Chiwalo
 Baadhi ya wageni na waandishi wa habari wakiwa nyumbani kwa Rachel Sharp wakiomba
 Walioko mbele ni mama wa Rachel Sharp (kulia) akiwa na mwanae Rachel Sharp wakati wa utambulisho
 Rachel Sharp akisoma Press Release kwa waandishi wa habari na bloggers
 Master Prophet Machibya akipokea mic kutoka kwa MC Ritha kwaajili ya kuanza zoezi la kuombea albamu ya Rachel Sharp
 Mtangazaji wa Clouds na blogger Samsasali akifanya mahojiano na Upendo Kilahiro
 Rachel Sharp akimchezea Mungu wetu kwa furaha
 Master Prophet Machibya akifanaya mahojiano kuhusiana na ujio mpya wa Rachel Sharp
 Master Prophet Machibya wakiwa na Rachel Sharp katika picha ya pamoja baada ya kuiombea albamu
 Bloggers Rulea Sanga (kulia) na Samsasali wakicheki matukio
 Wakati wa msosi



 Mtangazaji wa radio, Erick Brighton (kulia)

 Mchekeshaji Chavala akiwa katika mawasiliano

 Rachel Sharp akiwapongeza watu waliofika kwa makofi
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimchukua mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania, Upendo Kilahiro wakati akaiimba.
 Rachel akitambulisha wazazi wake

 Rachel Sharp na Nabii Machibya wakati wa kuombea albamu mpya
 Chavala akiwavunja mbavu waliofika katika hafla hii.




Ma Bloggers Kulia Kutoka Shalom na kushoto Kutoka Rejoice ndani ya eneo la tukio

Upendo Kilahiro na Rachel Sharp
 Ze Blogger Samsasali na Kilahiro
 Upendo Kilahiro akiwa anafanya performance siku ya leo nyumbani kwa Rachel
---------------------------------------------------
PICHA NA HABARI ZIMEANDALIWA NA
Rulea Sanga
Creative Director and Graphic Designer
RUMAFRICA
Mob: +255 715851523
Email: rumatz2012@gmail.com

HABARI KUHUSU MTANGAZAJI WA RADIO UINGEREZA BBC ZAWADI MACHIBYA


KWA TAARIFA YAKO: ZAWADI MACHIBYA MTANGAZAJI NYOTA ALIYEWEKA REKODI NCHINI

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu.


Zawadi Machibya akiuliza swali kwa waziri mkuu mh. Mizengo Pinda (hayupo pichani) alipotembelea nchini Uingereza mwaka jana.

Katika KWA TAARIFA YAKO hii leo tuko na mtangazaji maarufu nchini na ukanda wa Afrika mashariki . Huyu si mwingine bali ni Zawadi Machibya, mtangazaji wa Shirika la utangazaji la Uingereza BBC tokea mwaka 2009 mpaka hivi sasa (vijana wa sasa wanasema Jembe), akisikika kupitia idhaa ya Kiswahili ya shirika hilo. Awali alikuwa mwajiriwa wa Shirika la utangazaji Tanzania toka mwaka 1994 hadi 2000 akianzia Radio Tanzania, enzi hizo ikiitwa (RTD), kisha kuanzia mwaka 2000 hadi 2008 kwenye runinga ikiitwa TVT, kabla haijabadilishwa kuwa TBC ambako amefanya vipindi mbalimbali kama vya Mahojiano, Tuambie, mijadala, vipindi vya wanawake na watoto, Bunge, vipindi vingine vikiwemo kuripoti matukio, kuandika makala na kadhalika.


Milton na Gift watoto wa Zawadi katika pozi.

Zawadi, mama wa familia ya watoto watatu, Milton, Gift na Godson ana mengi ambayo jamii haiyajui labda kwa watu wake wa karibu. sasa KWA TAARIFA YAKO Zawadi ndiye aliyeweka rekodi nchini kwa kuwa Rais wa kwanza mwanamke katika serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu nchini akiwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza (SAUT) Pia ni mmoja wa waanzilishi wa umoja wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu (TAHLISO). Licha ya hayo, Zawadi ameokoka na anampenda Yesu, akiwa pia amefanya huduma mbalimbali vijijini kabla ya kuingia ulimwengu wa habari, lakini ilikuwaje mpaka akaamua kuingia kwenye media?

"Niliipenda kazi hii tangu mtoto. Nilipenda lugha hata kusomea masomo ya (HGL), na kuwapasha watu habari, matukio, kuwapa taarifa. Nimemaliza shule, JKT( ambako akiwa mafunzoni alikuwa mchungaji akisaidiana na mwenzake anayefahamika kwa jina la Busara).Halafu nikaanza kazi ya Injili vijijini (Singida) semina, mikutano ya nje uimbaji (Huduma Band na akina Pastor Abel Orgenes, Grace Msusu, Magreth, Elia Kisigila, Elisante,Arthur na wengine.) Muda umefika natakiwa chuo, lakini naona tangazo la kazi Daily News-kwa Radio Tanzania, SHIHATA, Idara ya Habari Maelezo. Nika-apply lakini kwakuifanyia maombi mazito barua yangu ya kuombea kazi, nikaziombea barua, nikazituma. Halafu nikaendelea na huduma, wakati Fernandus Venon na huduma ya SOM-School of Ministry ya Morris Cerullo, wakija Singida, nikafanya kazi. Baadaye napokea barua ya kuitwa kwenye usaili na kisha kupata kazi radio Tanzania nikiwa MADHABAHUNI" amebainisha Zawadi.


Watoto wa zawadi, Gift pamoja na Godson.

Lakini vipi kuhusu wokovu na kazi yake anasemaje ''Inatangulia IMANI, ndiyo inanifanya hivi nilivyo. Kuna mamlaka iliyo kuu, ambayo inasimamia na kuongoza kila ninachofanya. Naamini uzima unaanzia rohoni, halafu unashuka kwenye nafsi halafu mwilini. Kama roho haina uongozi HASA WA KIMUNGU, ni vigumu kuvuka majaribu, changamoto, majukumu, na ufahamu -(Knowledge) Chanzo ni kumcha Mungu). Pili, macho ya rohoni. Giza duniani kubwa bila msaada wa macho ya rohoni, si rahisi kuona''.


Zawadi akimwelekeza kitu bwana Julius Malema mwanasiasa kijana maarufu wa Afrika ya kusini alipofika ofisi za BBC London mapema mwaka jana.

"Utakumbuka kuwa Yesu aliwaonya watu juu ya ‘kuwa macho na waandishi wa habari na …..wengineo.’ La msingi ni kuwa uandishi na utangazaji ni kazi ya watu. Unawapa nini, unatangaza nini na je WEWE UNAJUA NINI KUHUSU WATU NA MAISHA YAO KISIASA, KIJAMII, KIUCHUMI, KIMAISHA, UTAMADUNI WAO, IMANI ZAO, n.k.Na unapofika ngazi ya kimataifa kama hivi hii ya BBC, wigo wako kiuelewa lazima uendane na hadhi ya chombo unachokitumikia. Mfano kujua nani anafanya nini wakati gani, kwa manufaa ya nani na kwa kiwango gani na mengine mengi! Hapa utaleta mataifa makubwa ya Ulaya, Marekani, China, Afrika kama Bara, viongozi wake na bila kusahau majanga yanayoikumba dunia likiwemo ‘kudorora kwa uchumi na mzozo kuhusu sarafu ya Euro’ utaona kuwa maeneo mengine kama yanaoendelea huko Australia, hali ikoje na mengine". amesema Zawadi.

KWA TAARIFA YAKO kuna watu mbalimbali ambao wamechangia mafanikio yake katika ulimwengu wa habari, ambapo ameiambia GK kuwa ''Kwa upande wa kazi, ni mzoefu na mwalimu mzuri. Niko kwenye taaluma hii kwa karibu miaka ishirini sasa. Watu wa muhimu kuwakumbuka hapa ni Mama Edda Sanga ndiye aliyenifundisha kazi (RTD), lakini na wengine wazoefu wakiwemo.

Unaweza kumsikia Zawadi vyema kupitia vipindi vya Dira ya dunia, Leo Afrika na vinginevyo kupitia Idhaa ya Kiswahili ya BBC ikikutangazia moja kwa moja kutoka jijini London nchini Uingereza. Zawadi anayo mengi ya kueleza, GK itamtafuta tena kwa maongezi zaidi.


Zawadi Machibya pamoja na John Solombi (ndani ya studio) wakiwa katika moja ya studio zilizokuwa katika jengo la zamani la BBC, Bush House jijini London, hapa ni kipindi cha ''Dira ya dunia''

Zawadi mkono wa kushoto akiwa na John Solombi katika Dira ya dunia.

Zawadi akiwajibika kumtumikia Mungu katika moja ya mikutano vijijini.


Zawadi enzi hizo akiwa katika huduma moja ya kijiji mkoani Morogoro.


Zawadi akiwa pamoja na mumewe Apostle Machibya. picha ya enzi hizo.

Haya mdau wetu hiyo ni ''KWA TAARIFA YAKO'' hii leo kama ulikuwa hujui, vinginevyo tukutane wiki ijayo au wasiliana nasi kwa barua pepe gospelkitaa@post.com. BARIKIWA
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...